Trump: Marekani Haijalenga Kuchukua Uranium ya Iran ‘Kwa Sasa’
2026-03-14 - 00:47
Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa kwa sasa Marekani haijalenga kufanya operesheni ya kuchukua uranium ya Iran, ingawa alionyesha kuwa hatua hiyo inaweza kuwa chaguo katika siku za mbele. Akihojiwa na Fox News Radio kwenye kipindi cha The Brian Kilmeade Show, Trump alisema:“Siyo lengo letu kwa sasa, lakini wakati fulani inaweza kuwa chaguo.” Matamshi haya yanajiri huku mvutano wa kijeshi na kisiasa kati ya Marekani na Iran ukiendelea, na mashirika ya kimataifa ya nishati na usalama ya kuangalia mradi wa nyuklia wa Iran.
Share this post: