TheTanzaniaTime

Tazama Ujasiri wa Binti wa Kilimanjaro Girls Mbele ya Waziri Mkuu – Video

2026-02-22 - 09:16

Binti mmoja wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kilimanjaro ameonyesha ujasiri mkubwa alipata nafasi ya kuzungumza hadharani mbele ya Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, katika hafla iliyofanyika Siha mkoani Kilimanjaro. Katika hotuba yake, mwanafunzi huyo alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi zake katika kuinua sekta ya elimu nchini. Alitaja kwa msisitizo manufaa ya programu ya Samia Scholarship, akieleza jinsi ilivyowapa fursa wanafunzi wenye ufaulu mzuri kuendelea na masomo yao ya juu bila vikwazo vya kifedha. Ujasiri na umahiri wake wa kuzungumza mbele ya viongozi wakuu uliwavutia wengi waliohudhuria hafla hiyo, huku akipokea pongezi kwa kuwakilisha vyema wanafunzi wenzake.

Share this post: