TheTanzaniaTime

Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) Wagomea Uamuzi wa CAF, Kukata Rufaa

2026-03-18 - 09:24

Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) limekosoa uamuzi wa CAF kuwatangaza kupoteza mechi ya fainali ya AFCON 2025 , na hivyo ushindi wa mezani wa mabao 3–0 kutolewa kwa Morocco . FSF limeahidi kupeleka rufaa kwa Mahakama ya Michezo (CAS) huko Lausanne. Katibu Mkuu wa FSF, Abdoulaye Sow, amesema: “Kombe halitaondoka nchini. Senegal ina haki, na ushindi upo upande wake.” Wachezaji pia walionyesha hisia za hasira na uchungu: Idrissa Gana Gueye alisisitiza kuwa vyeo na vikombe vinaisha, lakini heshima ya mashabiki na jamii ndiyo muhimu zaidi. El Hadji Malick Diouf, ambaye alihusika kwa kosa la penati, aliongeza: “Kombe linashindaniwa uwanjani, sio kwa barua pepe.” Habib Diarra aliweka picha akiwa na kombe kwenye Instagram, kuonyesha kwamba timu haiwezi kukata tamaa. Bodi ya Rufaa ya CAF ilitangaza kwamba Senegal imepoteza fainali, na matokeo kuandikwa kama 3-0 kwa Morocco. Shirikisho la Soka la Morocco limekubali uamuzi, lakini limeeleza kwamba rufaa yao ilikuwa juu ya kutekeleza kanuni za mashindano pekee, si kupinga utendaji wa timu yoyote.

Share this post: