TheTanzaniaTime

Serikali Yatangaza Ajira 142 NAOT kwa Fani Mbalimbali

2026-01-25 - 21:09

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, kwa niaba ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT), anakaribisha maombi ya kazi kutoka kwa Watanzania wenye sifa, uwezo na nia ya kufanya kazi serikalini kujaza nafasi 142 kama zilivyoainishwa hapa chini. NAFASI ZILIZOTANGAZWA BONYEZA HAPA >>>OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI 1. Mkaguzi Daraja la II – Nafasi 121 Sifa: Shahada ya Kwanza ya Uhasibu, Uhasibu na Fedha, Uhasibu na TEHAMA, au Uhasibu wa Sekta ya Umma kutoka vyuo vinavyotambuliwa na Serikali. Ngazi ya Mshahara: SAIS E 2. Afisa Habari Daraja la II (Graphic Design) – Nafasi 1 Sifa: Shahada ya Multimedia Technology au Graphic Design Ngazi ya Mshahara: TGS D 3. Afisa Habari Daraja la II (Uandishi wa Habari) – Nafasi 1 Sifa: Shahada ya Uandishi wa Habari au Mawasiliano ya Umma Ngazi ya Mshahara: TGS D 4–19. Wakaguzi Daraja la II (Fani Mbalimbali) Nafasi zinapatikana katika fani zifuatazo: Udaktari wa Mifugo Famasia Afya ya Jamii Ustawi wa Jamii Uhandisi wa Maji na Usafi wa Mazingira Umwagiliaji na Rasilimali za Maji GIS / Geoinformatics Biomedical Engineering Thamini ya Ardhi Land Use Planning Electrical Engineering Quantity Survey Civil Engineering Architecture Actuarial Science Tax Management Ngazi ya Mshahara: SAIS E (Waombaji wahakikishe wamesajiliwa na bodi husika za kitaaluma) MASHARTI YA JUMLA Mwombaji awe Raia wa Tanzania, umri usiozidi miaka 45 Vyeti vyote viwe vimethibitishwa na Mwanasheria/Wakili Waombaji waliosoma nje ya nchi wahakikishe vyeti vimehakikiwa na TCU/NECTA/NACTE Waombaji waambatishe CV, cheti cha kuzaliwa, vyeti vya elimu na kitaaluma Matokeo ya muda (Result Slips) hayakubaliki Mwisho wa kutuma maombi: 24 Januari, 2026 NAFASI ZILIZOTANGAZWA BONYEZA HAPA >>>OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI

Share this post: