TheTanzaniaTime

Rais Trump: Viongozi wa Iran Wanataka Tuzungumze ‘Wamechelewa’

2026-03-03 - 16:07

Rais wa Marekani, Donald Trump Rais wa Marekani, Donald Trump, ameendelea kuishambulia Iran kwa maneno makali akidai kuwa viongozi waliosalia wa Tehran sasa wanataka mazungumzo, lakini “muda umechelewa.” Kupitia akaunti yake ya Truth Social, Trump aliandika: “Ulinzi wao wa anga, Jeshi la Anga, Jeshi la Wanamaji na uongozi wao umeondoka. Wanataka kuzungumza. Nilisema ‘Too Late!’ (wamechelewa) Kauli hiyo imekuja huku mapigano kati ya Marekani, Israel na Iran yakiingia siku ya nne, na Trump akionya kuwa “mapigo makali zaidi bado yanakuja.” Pia ameahidi kulipiza kisasi kufuatia shambulio la ndege zisizo na rubani dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini Riyadh, Saudi Arabia. Mashambulizi ya anga ya Marekani na Israel yamelenga mkutano wa wanazuoni wa dini wa Iran waliokuwa wakijadili suala la kiongozi mkuu ajaye wa nchi hiyo. Jeshi la Iran limedai kushambulia Israel na kituo cha kijeshi cha Al-Udeid nchini Qatar, kinachotajwa kuwa kambi kubwa zaidi ya Marekani katika Mashariki ya Kati. Mabaki ya ndege isiyo na rubani iliyozuiwa yalisababisha moto katika kiwanda cha kusafisha mafuta nchini United Arab Emirates. Haya Ndiyo Yanayoendelea Hadi Sasa: Saudi Arabia imelaani shambulio la drone dhidi ya ubalozi wa Marekani mjini Riyadh, ikilitaja kuwa “lisilo na sababu” na “la woga.” Israel imeripotiwa kulenga ofisi ya rais wa Iran mjini Tehran na pia kupeleka wanajeshi kuingia Lebanon kuchukua nafasi mpya dhidi ya kundi la Hezbollah. Trump amemshutumu Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, kwa kuhatarisha uhusiano maalum wa Marekani na Uingereza baada ya kutomuunga mkono kikamilifu kuhusu vita na Iran. France imetuma ndege za kivita juu ya UAE na meli za kivita kulinda Cyprus, ambako kambi ya kijeshi ya Uingereza ilishambuliwa. Jenerali wa Iran ameonya kuwa Tehran “itachoma kila meli” katika Strait of Hormuz, hatua inayozua hofu ya kupanda kwa bei ya mafuta duniani. United Nations imethibitisha kuwepo kwa uharibifu katika kituo cha kurutubisha urani cha Natanz kufuatia mashambulizi ya Marekani na Israel. Mvutano huo unaendelea kuongezeka huku jumuiya ya kimataifa ikionya kuhusu hatari ya mzozo huo kugeuka vita kamili vya kikanda, jambo ambalo linaweza kuathiri usalama wa nishati na uchumi wa dunia kwa ujumla.

Share this post: