Rais Samia Kuhusu Waziri Salum – ”Acheni Midomo ya Uongo”
2026-02-09 - 10:09
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Februari 09, 2026, amewaapisha viongozi mbalimbali aliowateua katika hafla iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam. Miongoni mwa viongozi walioapishwa ni Waziri Salum, ambaye ameapa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara. Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Samia amegusia minong’ono iliyokuwepo miongoni mwa wananchi kufuatia uamuzi wake wa kumtoa Waziri Salum Ikulu, hatua iliyozua maswali kuhusu sababu ya mabadiliko hayo, ikizingatiwa kuwa wamefanya kazi kwa karibu kwa muda mrefu. Rais Samia ameeleza kuwa mabadiliko anayoyafanya katika teuzi zake kwa viongozi aliowahi kufanya nao kazi yanalenga kuwakuza, kuwajengea uzoefu mpana wa uongozi na kuwaandaa kwa majukumu makubwa zaidi. Amefafanua kuwa hatakuwepo Ikulu milele, na kwamba viongozi watakaomfuata wanaweza kuja na timu zao wenyewe, hivyo ni muhimu kwa viongozi wa sasa kupata fursa mbalimbali za kiuongozi mapema