TheTanzaniaTime

Mwanachuo Mwaka wa Kwanza Mbaroni Kwa Kusafirisha Dawa Za Kulevya

2026-02-10 - 14:29

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa wanne ambao ni Wilfred Komba, miaka 24, Mwanachuo mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu cha Iringa, Lenad Shamba maarufu Paulo, miaka 21, mkazi wa Tarime Mkoa wa Mara, James Mwakalebela, miaka 26, mkazi wa Ngonga – Kyela na Joseph Mkwara maarufu Aliki, miaka 26, mkazi wa Kyela kwa tuhuma za kusafirisha dawa za kulevya aina ya Bhangi yenye uzito wa Kilo 45 na Gramu 785 katika nyakati tofauti. Watuhumiwa walikamatwa wakiwa na dawa hizo za kulevya zikiwa kwenye mabegi matatu na mifuko miwili ya sandarusi wakizisafirisha kwa mabasi ya abiria kutoka Mbeya kuelekea Dar es Salaam. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa waliingiza dawa hizo nchini kutokea nchi jirani.

Share this post: